Mapenzi salama
Kama unahisi uko tayari kufanya mapenzi, au tayari unashiriki katika ngono, ni vyema kuchukua tahadhari. Hakikisha katika harakati zako za kufanya mapenzi, unajali afya yako kwa kufanya ngono iliyo salama.
Inaweza kuwa vigumu, na jambo unalolionea haya kujadiliana na mapenzi wako, swala la uwezekano wa kuambukizwa magonjwa ya
zinaa, na kutumia njia za kuzuia mimba.
Lakini kulikwepa swala hilo kwaweza kumaanisha kuhatarisha afya na maisha yako kwa jumla. Kufanya mapenzi salama , maana yake
ni kutafakhari maswala hayo na kisha kuchukua hatua zifaazo.
Punyeto Ni nini?
Kufanya au kupiga punyeto, ni tendo la kutomasa sehemu zako mwenyewe za siri ili kujisisimua kimapenzi.
Kwa hivyo katika kupiga punyeto hamna hofu ya kuambukizwa magonjwa yanayosambazwa kupitia ngono, kwani haimshirikishi mtu
mwengine.
Punyeto ni toshelezo kamili la kimapenzi kama utatumia njia mbali mbali za kujitomosa na kujipa papasa ya kujistarehesha.
Hakuna mtu anayezaliwa akijua jinsi mwili wake unavyoitikia msisimko wa kimapenzi. Inakubidi kujifunza kwa majaribio salama.
Na, kwa vile kila mtu yuko tofauti, njia nyengine ya kujua jinsi unavyoweza kumstarehesha mpenzi wako, ni kujifunza kutoka
kwako mwenyewe.
Shughulika zaidi na sehemu ambazo zinasisimka kwa urahisi.
Unaweza kufikia kilele cha starehe yako kwa kuitomasa tomasa mboo au kisimi, lakini kutakupa hamu kubwa na ashiki, na kufikia
kutoshelezwa vya kutosha, kama utapapasa pia sehemu nyenginezo za mwili wako.
Kwa nini punyeto huonekana kuwa makosa?
Msimamo wa dini nyingi na watu wengi ni kuwa punyeto ni dhambi, mwiko, jambo lililokatazwa, jambo lisilokubalika kabisa.
Lakini wanasanyansi wanasema ni jambo salama kiafya na dhana zilizopo kulihusu, ni imani za kibinafsi na chaguo la mtu.
Wanaume wengi na wanawake hupiga punyeto maishani mwao, kwa sababu huwafanya wakajisikia vizuri na huondoa dhiki za mihemko
ya kimapenzi bila kujiingiza katika ngono na mtu mwengine.
Pia hofu ya kuambukizwa magonjwa ya zinaa, ikiwemo virusi vya HIV ni kichocheo tosha kinachopelekea baadhi ya watu kupiga
punyeto.
Njia za kuzuia mimba
Dawa au vifaa vya uzazi ni baadhi ya taratibu zinazotumiwa kuzuia mimba kutungwa. Ikiwa msichana au wanamke atafanya mapenzi
pasi na kutumia mojawapo ya mbinu hizo basi, kuna uwezekano wa theluthi moja kwamba atapata mimba.
Hata hivyo aina yoyote ya kuzuia mimba utakayoichagua ni lazima itumiwe kama ilivyoagizwa, ili kuleta matokeo ya hakika.
Baadhi ya njia hizo kama vile kutumia kondom wakati wa ngono, pia kwa kiasi fulani humpa mtu kinga dhidi ya maambukizo ya
virusi vya HIV, na magonjwa mengine yanayoathiri afya ya uzazi.
Kwa vile mbinu za kuzuia uzazi ni za aina
tofauti tofauti, ni muhimu basi uchague kwa makini ile inayokufaa.
Utapata usaidizi
wa kitaalam kama utashauriana na daktari wako, au pata
usaidizi katika kituo cha kwenu cha upangaji uzazi, au kituo cha vijana.
Mbinu za kuzuia mimba (Contraception)
Hivi ni vifaa au dawa zinazotumiwa kwa minajili ya kuzuia mimba kutungwa wakati wa kufanya ngono.
Kuna zile zinazotumiwa kwa mda mfupi na nyengine kwa mda mrefu. Nyengine hufanya kazi papo hapo na nyengine huitaji maandalizi
ya mda.
Kondom au tembe maalum ndizo njia bora zinazojulikana zaidi za kuzuia mimba.
Kondom au tembe maalum ndizo njia bora zinazojulikana zaidi za kuzuia mimba.
Pia kondom zina manufaa bora zaidi zinapotumuwa kwani mbali na kuzuia mimba zinapotumika kama inavyopaswa zinaweza pia kumkinga
mtu asiambukizwe vurusi vya HIV, na magonjwa mengine ya zinaa.
Tuangalie kwanza vifaa vya kuzuia mimba.

Moja ya mbinu bora na rahisi za kuzuia mimba, ni kuweka kizuizi, kwa lengo kuwa mbegu ya mwaname na ile mwanamke zisikutane. Kwa maana hiyo kifaa maalum kinaweza kuwekwa katika njia inayotumiwa na mbegu ya kiume ndio isilifikie yai la mwanamke.
Baadhi ya vifaa hivi (hasa kondom) pia vinaweza kukinga kuambukizwa virusi vya Ukimwi, na magonjwa mengine ya kuambukizana
kupitia ngono.
Kuna aina kadhaa za vifaa vya kuzuia mimba. Kondom za wanaume na zile za wanawake ndio vifaa vinavyofahamika zaidi, hata
hivyo kuna pia vifaa vyenginevyo viitwavyo diaphragm na caps kwa kimombo ambavyo vinaweza kutumiwa na wanawake.
Kondom za wanaume: Hivi
hutengenezwa kutokana na aina maalum ya mpira uitwao latex, au plastiki
nyembamba. Kondom ya mwanaume huvaliwa kwenye
uume iliyosimama, tena kabla ya uume kuingizwa ukeni.
Ikitumiwa kama inavyotakikana inakadiriwa kuzuia mimba kwa asilimia
98.
Kwa kawaida kondomu hupatikana kwenye vituo au kliniki za upangaji uzazi, kwenye maduka ya madawa au hata maduka ya kawaida.
Kondomu za wanawake:
Halkadhalika hutengenezwa kwa mipira laini ya latex au plastiki
nyembamba maalum. Huvaliwa ndani ya uke, huku sehemu iliyowazi
ikichomoza nje kidogo. Kwa kawaida kondom za wanawake ni
ghali, na pia utendaji kazi wake unakadiriwa kuzuia mimba kwa asilimia
95.
Aina nyenginezo na vifaa vya kuzuia mimba huwa hazipendekezwi kwa vijana lakini ni vyema kuvijua.
Kuna aina nyenginezo za vifaa vya kuzuia mimba viitwavyo diaphragms na caps. Hivi hutengenezwa kutokana na kitu kiitwacho silicone au mpira laini maalum. Vikiwekwa ukeni hutumika kama
vizibo vya kuzuia mbegu za mwanamme kupenya hivyo basi haiwezi kukutana na yai la mwanamke.
Kwa kawaida caps ni ndogo kuliko
diaphragms lakini kwa vile wanawake pia wana maumbo tofauti, ni sharti
upate saizi utakayokutosha.
Hapa ni sharti upate usaidizi wa daktari wako, au muuguzi,
kuiweka.
Inapowekwa mahali pake ndani ya uke, iwe
diaphragm au cap, huziba kilango cha mfuko wa uzazi hivyo basi mbegu ya
mwanamme
haitapatanafasi ya kupita. Ukishaonyeshwa na daktari jinsi
ya kuipachika, baadae unaweza kuipachika mwenyewe kabla ya kufanya
mapenzi.
Kwa matokeo bora zaidi, diaphragms na caps hutumiwa pamoja na dawa iitwayo (spermicide) ambayo huuwa mbegu za uzazi za mwaname.
Hapo diaphragms au caps humpa mwanamke kinga dhidi ya mimba kwa asilimia kati ya 92 na 98.
Hata hivyo itachukua mazoezi ya muda ili kuvitumia itakikanavyo. Wakati mwengine pia hutumiwa na gel yake maalum lakini bado
havina hakikisho la asilimia moja kuzuia mimba.
Faida yake nyengine ni kuwa, kwa kiasi fulani, vinaweza kukinga dhidi ya magonjwa ya zinaa na saratani ya (cervix) lango la
nyumba ya uzazi.
Ikiwa wewe hutumia vifaa kama diaphragms au caps, au hata kondom, ni vyema kujipangia mapema ndio usikose akiba, ndio haitakuwa
karaha kuvitafuta pale unapovihitaji.
ITAENDELEA........
Source; www.bbc.com
Source; www.bbc.com
0 comments:
Post a Comment